BASHUNGWA ATUMIA HELIKOPTA KUKAGUA UREJESHAJI WA MAWASILIANO YA BARABARA YA DAR – LINDI.
Published on: 12 days ago
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akiwa kwenye Helikopta akikagua na kujionea kazi ya urejeshaji wa mawasiliano ya barabara ya Lindi – Dar es Salaam iliyoathiriwa na mvua iliyoambatana na Kimbunga Hidaya, leo tarehe 7 Mei, 2024.
Kazi hiyo ya urejeshaji wa miundombinu ya barabara na madaraja inaendelea kufanywa na timu ya wataalamu wa Wakala ya Barabara (TANROADS) na Makandarasi.
= = = = =
Unataka kutuma habari? Submit on tuma kwetu kupitia info@kigogomedia.com au WhatsApp 07000000